Trending

Parade la Ubingwa Yanga SC laandika Historia

Dar es Salaam: Parade ya ubingwa ya Yanga SC iliyofanyika Julai 4, 2026 imeingia kwenye historia kutokana na shamrashamra kubwa, burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali pamoja na muziki uliotolewa na DJ Zee, hali iliyovutia maelfu ya mashabiki wa klabu hiyo.

Katika parade hiyo, beki wa Yanga SC, Mohamed Hussen "Zimbwe Jr.", alikuwa na jukumu la kuwaongoza na kuwatambulisha wachezaji waliokuwepo nchini wakati wa sherehe hizo. Mashabiki walipata fursa ya kuwaona kwa ukaribu nyota wa timu hiyo waliokuwa kwenye msafara wa mabingwa.

Miongoni mwa wachezaji waliopokelewa kwa shangwe kubwa alikuwa kiungo Allan Okello, ambaye ameendelea kuonesha kiwango bora tangu alipojiunga na Yanga SC katika dirisha dogo la usajili la msimu wa 2025/26.

Aidha, mashabiki hawakumsahau kiungo Stephane Aziz Ki, Pacôme Zouzoua ("Pacôme"), ambaye anaendelea na matibabu kutokana na majeraha. Wapenzi wa soka na mashabiki wa Yanga walitumia fursa hiyo kumuombea apone haraka ili arejee uwanjani na kuendelea kuitumikia timu.

Yanga SC imehitimisha msimu kwa kutwaa ubingwa wa NBC Premier League kwa mara ya tano mfululizo, mafanikio yanayoendelea kuthibitisha ubora wa klabu hiyo katika soka la Tanzania.

Parade hiyo ilipita katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, ikiwemo Mtaa wa Msimbazi, eneo linalohusishwa na watani wao wa jadi, Simba SC. Wakati parade ya Yanga ikifanyika, mashabiki wa Simba walikuwa wamejikusanya kufuatilia fainali ya CRDB Federation Cup dhidi ya Azam FC.

Siku iliyofuata, Simba SC walifanya parade yao ya ubingwa baada ya kuichapa Azam FC kwa bao 1-0 na kutwaa CRDB Federation Cup, huku msafara wao ukipita pia katika eneo la Jangwani, makao makuu ya Yanga SC.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Contact Form